Alhamisi, 13 Agosti 2015







 MBIO ZA URAIS TANZANIA NA POMBE MAGUFULI.
Ni katika hali ya furaha na shangwe juu ya uteuzi wa mweshimiwa POMBE JOHN MAGUFULI kusimanishwa na rais JAKAYA MRISHO KIKWETE katika kugombea nafasi ya urais....2015


 


Hatimaye kile kilicho kuwa kinasubiriwa kwa muda mrefu katika mkutano mkuu wa  chama cha mapinduzi -CCM- mkoani DODOMA kimejidhihirisha .

Zilianza mbio na heka heka za makada wa chama cha mapinduzi kuchukua fomu na kila mmoja kutangaza kwa nafasi yake kuwania kugombea kiti cha uraisi ambapo katika makada hao waliokuchukua fomu walifikia arobaini na mbili (42).

Zoezi hilo liliendelea na hatimaye ikafika wakati wa kila mmoja kurudisha fomu za uraisi ambapo pia katika kurudisha fomu hizo makada thelatini na nane walirudisha fomu na wanne hawakurudisha fomu hizo.

katika mkutano huo wa CCM ulianza mchakato wa mchujo ili kupata tano bora ambapo katika mchujo huo walipatikana waanawake wawili na wanaume watatu.

Hata hivyo huko kote ni katika kinyang'anyiro ya kutaka kiti cha uraisi au kutia guu IKULU,watano hao waliye chaguliwa ni pamoja na aliye kuwa naibu katibu mkuu wa umoja wa mataifa (UN) Dakta ASHA ROSE MIGIRO,Balozi AMINA SALUMU ALI, Waziri wa ujenzi Dakta JOHN POMBE MAGUFULI, naibu waziri wa sayansi na teknolojia  mh.JANUARY YUSUF MAKAMBA,na waziri wa mambo ya nje BERNAD KAMILIUS MEMBE.

Mchakato wa kuendelea kutafuta nani atakae ipeperusha bendera ya CCM hatimaye taifa ukaendelea na kuwatafuta watatu ambao walipatikana,watau hao ni pamoja na Dakta,ASHAROZI MIGIRO,Balozi AMINA SALUMU ALLY na Dakta JOHN POMBE MAGUFULI.

Hatimaye ukafika wakati wa kumtafuta mmoja kati ya wale watatu kwa kupiga kura na wajumbe mbali mbali walioshiriki katika mkutano huo wa CCM ambapo alipatikana mmoja huyo naye ni Dakta JOHN POMBE MAGUFULI ndiye atakae peperusha bendera ya chama hicho katika kampeni za uraisi licha ya kuwepo kwa vyama mbalimbali vya upinzani.

Hata hivyo, kupatikana  kwa mgombea huyo kuwania kiti cha urais kutaleta chachu na tija kwa wananchi kuondokana na umasikini ambao umekua ni kiilio miaka mingi kwa wananchi wa TANAZNIA .