Ijumaa, 20 Februari 2015



KERO YA MAJI

CHEMBA

Wananchi wakijiji cha kata ya makorongo wilayani chemba mkoani Dodoma wameiomba serikali kuwasaidia kuondokana na kero ya maji ambayo imekua ikiwasumbua kwa muda mrefu na kuwalazimu wananchi hao kufuata huduma ya maji kwa umbali mrefu.

Mwenyekiti wa serikali ya kijiji hicho FATUMA KITAMBI amesema kuwa kero hiyo kwa sasa imekua sugu kutokana na ubovu wa mashine wanayoitumia katika uzalishaji maji,na wakati mwingine huwalazimu kukopa fedha kwa wadau na kuendesha shughuli za uzalishaji maji
 
Naye mganga mfawidhi wa kituo cha afya  cha makorongo bahati mohamedi amesema kuwa athari wanazoweza kupata wananchi kutokana na kutumia maji yasiyo safi na salama ni pamoja na kupata magonjwa ya mlipuko kama vile kuharisha damu na ukosefu pamoja na ukosefu wa maji.
www.halfanbinde.blogsport.com 
Hata hivyo wananchi hao wamesema kwamba changamoto ambazo hukumbana nazo ni pamoja na kutumia muda mwingi kutafuta maji badala ya kufanya shughuli za uzlishaji.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni