Ijumaa, 20 Februari 2015



MIKOPO

DODOMA

Wajasiriamalimkoani DODOMA wameiomba Serikali kushirikiana na taasisi mbalimbali za mikopo zitakazowasaidia kuwakopesha fedha kwa masharti nafuu  ili waweze kukopa na kujikwamua kimaisha.

Wakizungumza na TBC, baadhi ya wajasiriamali wanaojishughulisha na shughuli za useremala katika eneo la MAJENGO mjini DODOMA wamesema kuwa, taasisi nyingi za kibenki zimekuwa zikiangalia mali walizonazo wajasiriamali kabla ya kuwakopesha hatua inayowakwamisha kukopa katika benki hizo.

 Aidha  wajasiriamali hao wamesema  juhudi kubwa wanazozifanya ni pamoja na kuboresha bidhaa wanazozitoa katika uzalishaji ili ziwe bora kwa lengo la kuwavutia wateja.

 Tatizo jingine linalowakabili wajasiriamali hao ni pamoja na ukosefu wa vifaa vya kuzalishia bidhaa, upatikanaji wa  mitaji na mzunguko wa biashara kuwa mgumu.

Wametoa wito kwa vijana kujishughulisha kufanya kazi kwa bidii badala ya kukaa vijiweni na kupiga soga huku wakitegemea kuajiriwa serikalini.

Hakuna maoni:

Chapisha Maoni