Alhamisi, 26 Februari 2015

MAONI
  DODOMA

Wananchi mkoani DODOMA wameiomba serikali  kuandaa vifaa ,mapema kwenye vituo vya kujiandikishia  kwa wakati ili kuepusha usumbufu ambao utajitokeza kwa wananchi katiaka zoezi la uandikishaji katika daftari la kudumu la wapiga kura .
   Wakizungumza kwa nyakati tofauti wananchi wa mkoa wa DODOMA  wameeleza kuwa serikali inatakiwa kuaangalia mapema mapungufu mbalimbali ili katika mfumo unaotumika kwa sasa.
    Hata hivyo wameitaka serikali kuendelea kutoa elimu zaidi  ya matumizi ya mfumo unaotumika sasa katika zoezi la kijiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura ili kutokupoteza haki yao ya msingi ya kupiga kura.
     Mbali na hayo  akizindua  daftari la uboreshaji la wapiga kura mkoani NJOMBE wilaya ya MAKAMBAKO waziri mkuu wa TANZANIA  MIZENGO PINDA amewataka viongozi wa siasa kuwahamasisha wananchi kwa wingi kujitokeza katika zoezi la kijiandikisha katika daftari la kudumu la wapiga kura bila kujali itikadi za kisiasa.    



Hakuna maoni:

Chapisha Maoni